Chama cha Wafanyakazi wa Usafiri wa Anga kimesitisha mgomo wake uliovuruga safari za ndege katika viwanja vya ndege, kufuatia mazungumzo na serikali. Chama hicho kinasema wafanyakazi wataanza kazi tena na kushirikiana na usimamizi ili kurejesha shughuli za kawaida mara moja. Miongoni mwa maazimio yaliyofikiwa ni pamoja na kuondolewa kwa barua ya awali ya mwongozo wa Tume ya Mishahara na Malipo iliyotolewa Julai. Vigezo vipya sasa vitaongoza mazungumzo yanayoendelea kati ya pande hizo mbili.


DAVIS CHIRCHIR – STRIKE