Wanawake wawili walifariki baada ya boti ya watalii iliyokuwa imewabeba wageni na wafanyakazi kuzama katika Bahari ya Hindi karibu na Watamu, Kaunti ya Kilifi, polisi walisema. Tukio hilo lilitokea Jumapili,, yapata saa 4:30 jioni. Boti hiyo ilikuwa imebeba watalii, waongoza watalii na wafanyakazi katika safari ya kurudi Ufuoni wakati mawimbi makali ya bahari yalipoipiga, na kusababisha kuzama. Abiria hao walijumuisha watalii sita wa Italia.