Timu ya taifa ya voliboli ya wanawake, Malkia Strikers, ilijikatia nafasi katika robo fainali ya Mashindano ya Mataifa ya Afrika ya Wanawake ya 2026 baada ya kuishinda Nigeria 3-0 katika Uwanja wa Ndani wa Kasarani jana. Nigeria iliwafanya Kenya kutoa kijasho kwa seti ya ufunguzi, kabla ya wenyeji hatimaye kushinda 25-21. Kenya iliimarika na kushinda seti ya pili 25-17, kabla ya kunyakua seti ya tatu, 25-15.


 Wakati huo huo, Uganda iliishinda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 3-0, kabla ya Algeria kuilaza Senegal kwa tofauti hiyo hiyo. Cameroon inajiunga nao katika robo fainali baada ya kupata sare ya raundi inayofuata.



Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Kericho. Kisii na Kitale.

Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.