Tume ya Haki ya Utawala imetoa wito kwa taasisi za umma kuchukua hatua haraka kuhusu malalamiko, upatikanaji wa maombi ya taarifa na mapendekezo. Tume hiyo ilionya kwamba kuchelewa kwa majibu kunaweza kupunguza imani ya umma kwa serikali. Mwenyekiti wa tume hiyo Charles Dulo alisema taasisi za umma lazima ziende mbali zaidi ya kujibu tu mawasiliano na kuanzisha mifumo inayohakikisha malalamiko yanashughulikiwa, kutatuliwa na kutumika kuboresha utoaji wa huduma.
CHARLES DULO – NATURE