Hazina ya Biashara wa Wanawake imetoa wito wa kuongezwa kwa ufadhili ili kuiwezesha kusaidia vikundi vingi vya wanawake kufuatia ongezeko la mahitaji ya ufadhili wa bei nafuu wa kuanzisha na kupanua biashara. Mkurugenzi Mtendaji Rachael Musyoki alisema Shirika hilo linapokea idadi inayoongezeka ya maombi kutoka kwa vikundi vya wanawake wanaotafuta usaidizi wa kifedha, huku baadhi ya wanufaika waliopo pia wakitafuta mikopo ya juu. Musyoki alikuwa akizungumza wakati wa utoaji wa hundi zenye thamani ya Sh milioni 41.2 kwa vikundi 200 vya wanawake huko Kilifi.