Chama cha Wauguzi Nchini kimelaani madai ya kupelekwa kwa watu walioajiriwa kuvuruga maandamano ya amani ya wauguzi katika Kaunti ya Kisii. Katibu Mkuu Seth Panyako alisema wauguzi walioshiriki katika maandamano ya amani jana walikabiliwa na watu aliowaelezea kama wahuni, akiwashutumu polisi kwa kushindwa kutoa ulinzi wa kutosha. Chama hicho kilitoa wito wa uchunguzi ili kubaini kilichotokea na kuwatambua wale waliohusika na usumbufu huo.
PANYAKO MULUNDA - GOONS