Udhamini wa jumla wa Ligi Kuu ya Kenya kutoka kwa mdhamini wa taji la Sportpesa umeongezeka kutoka Ksh. milioni 85 misimu iliyopita hadi Ksh. milioni 90 msimu huu. Kati ya Ksh. milioni 90, 40% ambayo ni takriban Ksh. milioni 36 itaenda kwa shirikisho kugharamia gharama za utawala. Asilimia 60 iliyobaki karibu Ksh. milioni 54 itagawanywa sawasawa miongoni mwa vilabu 18 vya ligi, huku kila klabu ikipokea Ksh. milioni 3 kwa mwaka, ikimaanisha Ksh. 250,000 kwa mwezi.

 

Chama cha Soka cha Afrika Kusini jana kilitangaza kurejea kwa Pitso Mosimane kama kocha mkuu wa Bafana Bafana. Kocha huyo wa zamani wa Sundowns na Al Ahly anarudi kwa mara ya pili baada ya kuiongoza Bafana kuanzia 2010-2012, kabla ya kufutwa kazi. Anachukua nafasi ya meneja wa Ubelgiji Hugo Broos ambaye mkataba wake ulimalizika baada ya kombe la Dunia la mwezi Julai. Pitso atasaidiwa na Kabelo Rangoaga kama kocha wa utimamu wa mwili, na Musi Matlaba kama mchambuzi wa utendaji na data. Mosimane atamteua msaidizi wake hivi karibuni.

PITSO MOSIMANE - SAFA 



Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Kakamega, Eldoret na Kisumu.

Ili kupata habari zaidi temebelea tovuti ya radiojambo.