Mshambuliaji wa Cameroon Monique Ngock alitajwa kuwa mchezaji bora wa Mashindano baada ya Indomitable Lionesses kuishinda Malawi 3-0 katika Kombe la Mataifa ya Afrika la Wanawake jana usiku mjini Rabat. Wakati huo huo, Michaely Bihina wa Cameroon alishinda Golden Glove baada ya kutoruhusu goli mara nne katika mechi tano. Temwa Chawinga wa Malawi alishinda Golden Boot baada ya kuibuka mfungaji bora kwa mabao matano na pasi mbili. Timu ya wanawake ya Algeria iliyomaliza katika nafasi ya tatu ilishinda Tuzo ya Fair Play- Algeria.




Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Nanyuki, Meru na Isiolo.

Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.