Wingu la huzuni limetanda kijiji cha Kenyatta Farm katika eneo bunge la Gatanga Kaunti ya Murang'a baada ya wakaazi kuamkia mauaji ya kutisha ya ajuza mwenye umri wa miaka 90. Mwili wa Hannah Ndururu ulipatikana nje ya boma lake na ulikuwa na majeraha makubwa kichwani. Wakaazi, na jamaa walioshtuka walidai kwamba mzozo wa muda mrefu kuhusu umiliki wa ardhi unaweza kuwa ndio chanzo cha shambulio hilo.