Spika wa Seneti Amason Kingi anasema Kielelezo kipya cha Vipimo vya Utendaji wa Fedha za Kaunti kitaipa Bunge njia ya kutathmini jinsi kaunti zinavyosimamia fedha za umma. Kielelezo hicho kitafuatilia uidhinishaji wa bajeti, ukusanyaji wa mapato, matumizi ya maendeleo na utendaji wa ukaguzi. Kingi anasema matokeo hayo yatasaidia kutambua mapengo, kuhimiza usimamizi bora wa fedha na kuhakikisha rasilimali za umma zinaleta maendeleo yenye maana kwa raia.


AMASON KINGI – LAUNCH