FIFA inachunguza tabia ya vurugu ya wachezaji wa Argentina baada ya fainali ya Kombe la Dunia la mwaka 2026 baada ya kushindwa kwao 1-0 dhidi ya Uhispania Jumapili. Nahuel Molina wa Argentina alionekana akijaribu kumpiga kofi nahodha wa Uhispania Rodri wakati wa sherehe hizo. Leandro Paredes alimsukuma Eric Garcia kooni, na kumwangusha Gavi chini. Wadau wa soka pia wanaitaka Fifa kuiadhibu Argentina, kwa uchezaji mbaya baada ya kugeuka nyuma Uhispania walipokua wakipokea medali zao na kunyanyua kombe.

 Nahodha na meneja wa zamani wa Uingereza Kevin Keegan amefariki akiwa na umri wa miaka 75. Kifo cha Keegan kinakuja wiki saba baada ya kufichua kwamba alikuwa amegunduliwa na saratani. Wakati wa taaluma yake nzuri, Keegan alifurahia vipindi katika Scunthorpe United, Liverpool, Hamburg, Southampton na Newcastle. Mshindi huyo mara mbili wa Ballon d'Or baadaye aliongoza Newcastle, Fulham, Uingereza na Manchester City. Three Lions watasherehekea maisha ya Keegan watakapowakaribisha Uhispania katika mechi yao ya Ligi ya Mataifa ya Uefa huko Wembley mnamo Septemba.

Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Nairobi.

Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.