Usalama umeimarishwa kwa uchaguzi mdogo wa Ol Kalou leo, huku maafisa wawili wa polisi wakipelekwa katika kila kituo cha kupigia kura. Kamishna wa mlima kenya Joshua Nkanatha anasema upelekaji huo ulifanywa kwa ombi la IEBC ili kuhakikisha mchakato wa upigaji kura wa amani na utaratibu, akisisitiza kwamba maafisa hao wako pale kutoa usalama—si kuwatisha wapiga kura.