Kenya imetia saini makubaliano na kampuni kubwa ya dawa ya Marekani Pfizer ili kupunguza gharama ya kutibu saratani kadhaa kwa zaidi ya mara saba, huku baadhi ya dawa zikishuka kutoka Sh milioni 1 hadi chini ya Sh50,000 kwa kila mzunguko. Rais William Ruto alitangaza makubaliano hayo baada ya kukutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Pfizer Albert Bourla katika Ikulu ya Nairobi. Mkataba huo unashughulikia matibabu ya saratani ya matiti, tumbo, utumbo mpana, mapafu, kibofu na umio, pamoja na Leukemia, lymphoma na myeloma.