Sehemu ya Rironi-Naivasha ya Barabara ya Rironi-Mau Summit inatarajiwa kuwekewa lami kamili ifikapo Desemba, huku mradi unaoendelea wa kuunganisha sehemu mbili ukitarajiwa kupunguza msongamano wa magari na kuboresha usalama barabarani kwenye Norther Corridor yenye shughuli nyingi. Kulingana na meneja wa mradi Eric Yu, kazi za ujenzi zinaendelea vizuri na mwanakandarasi yuko mbioni kufikia tarehe ya mwisho ya Desemba.