Katibu Mkuu wa mambo ya kigeni Nje Korir Sing'Oei anatoa wito wa hatua kali za pamoja kutoka kwa nchi za Afrika katika kujadili madeni, akisema bara hili haliwezi tena kumudu kuwafikia wakopeshaji kama mataifa binafsi. Sing'oei anasema Afrika lazima zitumie msimamo wa pamoja wa AU kuhusu madeni, kuimarisha muungano wa wanaodaiwa unaopendekezwa na kuunga mkono Shirika jipya la Ukadiriaji wa Mikopo la Afrika. Anasema hatua zilizoratibiwa zitasaidia nchi za Afrika kupata ufadhili wa bei nafuu na kurejesha uhuru mkubwa wa kiuchumi.
KORIR SING’OEI – COUNTRIES