Mahakama imesimamisha kwa muda mazishi ya mfanyikazi wa KCB Rosemary Chemutai kufuatia mzozo kati ya mumewe na familia yake kuhusu ni nani anayepaswa kusimamia mazishi yake. Amri hiyo ilitolewa baada ya mumewe, Kevin Kimwatu, kwenda Mahakamani akitaka kuzuia kile alichokielezea kama mipango ya mazishi kufanywa bila yeye kushiriki. Kimwatu anasema alitengwa na mipango hiyo licha ya kuwa mume wa marehemu na baba wa watoto wao wanne.