Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino ametoa wito kwa Wakenya kuepuka uhuni na vurugu za kisiasa kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2027. Mbunge huyo, akimaanisha matukio ya hivi karibuni huko Homa Bay, anasema tofauti za kisiasa hazipaswi kuigawanya nchi. Amewasihi Wakenya kubaki wamoja na kuhakikisha uchaguzi ujao unafanyika kwa amani, akionya dhidi ya matumizi ya vurugu na magenge ya vijana kuendeleza maslahi ya kisiasa.

BABU OWINO – PEACE