Klabu za Ligi Kuu ya Kenya zimemwandikia Waziri wa Michezo Salim Mvurya wakitaka mkutano licha ya kesi inayoendelea mahakamani ambayo imechelewesha kuanza kwa msimu wa KPL wa 2026/27. Katika barua iliyoandikiwa waziri huyo, vilabu, kupitia uongozi wa Ligi Kuu ya FKF na wenyeviti wa vilabu wameomba mkutano na Mvurya ili kujadili njia ya kusonga mbele. Vita vya kushuka daraja na kupanda daraja kati ya Kariobangi Sharks na Mombasa United vinatishia mrundikano wa mechi huku AFCON ya 2027 pia ikiwa njiani.
Gor Mahia imeimarishwa na kurejea kwa mshambuliaji Patrick Essombe kutokana na jeraha la kifundo cha mguu alilopata nchini Rwanda wakati wa Kombe la CECAFA mapema mwezi huu. Mcameroon huyo sasa anapigania uteuzi katika kikosi. Wakati huo huo nahodha wa KO’gallo Sylvester Owino pia anatarajiwa kurudi mwezi ujao kutokana na jeraha la mguu.
Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Nairobi, Narok na Kajiado.
Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.