Rais William Ruto anatarajiwa kuzindua sare mpya ya Huduma ya Polisi ya Kenya leo wakati wa sherehe ya kukabidhi sare hiyo katika Chuo cha Mafunzo ya Polisi cha Kiganjo huko Nyeri. Mkuu wa Polisi Douglas Kanja alisema sare hiyo inafuata mapendekezo kutoka kwa zoezi la ushiriki wa umma la mwaka 2023. Maafisa huduma ya polisi wataanza kuivaa wiki ijayo, huku mabadiliko hayo yakikusudiwa kuongeza ari na utoaji wa huduma.

DOUGLAS KANJA – UNIFORMS