Kenya imethibitisha tena kujitolea kwake kufanya kazi na nchi za Afrika kuzuia, kugundua na kukabiliana na vitisho vya afya vinavyovuka mipaka. Akizungumza huko Addis Ababa, Ethiopia, Katibu wa Afya ya Umma Mary Muthoni alisema nchi lazima ziimarishe ushirikiano kwa sababu mkurupuko ya magonjwa inaweza kuenea haraka nje ya mipaka. Mkutano huo ulishuhudia kutiwa saini kwa Mkataba wa Ushirikiano wa Mpakani na uzinduzi wa akiba ya chanjo ya Mpox ili kuongeza maandalizi ya dharura.