Wadau wa elimu wametakiwa kwenda zaidi ya matamko ya sera na kuzingatia matokeo yanayopimika na endelevu. Akizungumza katika Mkutano wa pili wa Elimu wa Kanda wa EAC unaoendelea jijini Nairobi, Katibu wa Elimu Nelson Sifuna alisema elimu ya msingi ndiyo msingi wa kujifunza kote kunakofuata na mabadiliko ya kijamii na kiuchumi. Sifuna ametoa wito wa utekelezaji imara wa sera za elimu, akisema ahadi lazima zibadilishe kuwa maboresho yanayoonekana madarasani na matokeo bora ya kujifunza kwa watoto.

NELSON SIFUNA – EDUCATION