Waziri wa Kilimo Mutahi Kagwe anasema Kenya inaweza kufungua sekta ya nyama yenye thamani ya Sh bilioni 397 kupitia kuongeza thamani, uwekezaji na mauzo ya nje ya bei ya juu. Akizungumza katika Maonyesho ya Nyama ya Kenya 2026, Kagwe alisema Kenya ilizalisha tani elfu 613,627 za nyama mwaka wa 2024. Alionya kwamba kusafirisha wanyama hai nje kunamaanisha kusafirisha ajira nje, akihimiza nchi kusindika, kuweka chapa na kusafirisha bidhaa zaidi za nyama nje.
MUTAHI KAGWE – MEAT