Viongozi wa dini wanatarajiwa kukutana jijini Nairobi asubuhi ya leo kwa ajili ya jukwaa la kitaifa la mashauriano kuhusu uchaguzi wa amani, huku maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2027 yakiongezeka kasi. NCIC kwa ushirikiano na Baraza la Dini Mbalimbali la Kenya na World Vision, wataandaa jukwaa hilo ili kuimarisha ushirikiano na kukuza uchaguzi wa amani. Jukwaa hilo linakuja siku moja baada ya NCIC kuzindua ramani yake ya kuelekea uchaguzi usio na vurugu wa 2027, inayoitwa Uchaguzi Bila Noma.