Rais William Ruto anasema Msitu wa Mau umehakikishwa baada ya serikali kutoa hati miliki ya msitu huo. Akizungumza wakati wa ziara yake ya maendeleo huko Narok, Ruto alisema msitu huo hautatumika tena kama suala la kisiasa. Alisema serikali pia imetoa hati miliki kwa karibu wakaazi wote wanaoishi karibu na msitu huo. Ruto aliongeza kuwa mipango inaendelea ya kuulinda msitu huo kwa uzio.