Seneta wa Busia Okiya Omtatah ameliomba baraza la kitaifa la mitihani KNEC kufichua maelezo ya ununuzi na uchapishaji wa vifaa vya mtihani wa KCSE, KJSEA na KPSEA ya mwaka 2026. Anataka tume hiyo itoe taarifa kuhusu mchakato wa ununuzi, ikiwa ni pamoja na mbinu iliyotumika, wazabuni, vigezo vya tathmini, mwanakandarasi aliyefanikiwa, thamani ya mkataba, malipo, umiliki na uwezo wa kampuni iliyopewa kazi hiyo.