Maafisa wa Chama cha Liberty National Democratic Alliance (LINDA) wanasisitiza kwamba wao ndio wamiliki halali wa jina na utambulisho wa chama hicho huku kukiwa na mzozo kuhusu usajili wa Linda Mwananchi. Akizungumza katika makao makuu ya chama hicho huko Kiambu, kiongozi wa chama hicho Phanesio Thuku alisema LINDA ilianza usajili mnamo Novemba mwaka 2024 na ina uanachama wa kitaifa. Chama hicho kilituhumu Linda Mwananchi kwa kuingilia jina lake lililosajiliwa, alama na utambulisho, kikiapa kuchukua hatua za kisheria kulinda maslahi yake.
PHANESIO THUKU – LEGITIMATE