Mwenyekiti wa IEBC Erastus Ethekon amewasihi watu wazima na viongozi wa kisiasa kuwashauri na kuwahamasisha vijana kuhusu uhalisia na masomo ya migogoro ya uchaguzi uliopita. Ethekon anabaini kuwa wengi wa wapiga kura na raia vijana waliopiga kura kwa mara ya kwanza walikuwa watoto wachanga au ambao hawajazaliwa wakati wa vipindi vya kihistoria vya machafuko, wanaweza kukosa muktadha wa moja kwa moja kuhusu athari kubwa ya vurugu za uchaguzi, hivyo basi haja ya mwongozo wa kulinda utulivu wa kitaifa.
ERASTUS ETHEKON – SENSITIZE