Wapelelezi huko Kandara, Kaunti ya Murang’a, wameanzisha uchunguzi baada ya mwili wa mwanamume wa makamo kupatikana kando ya barabara ya Kiranga-Kahaini. Mwili huo ambao ulikuwa na jeraha la risasi kichwani uligunduliwa baada ya mkaazi mmoja kupewa taarifa na jirani. Maafisa wa polisi walitembelea eneo la tukio na kuanza uchunguzi. Kwingineko, mwanamume mmoja alipatikana amefariki akiwa na majeraha makubwa shingoni na mkono wa kulia katika shamba moja huko Kasemeni, Kaunti ya Kwale, katika kile ambacho polisi wanashuku kuwa mauaji. Maafisa wa DCI walifika katika eneo hilo huku uchunguzi ukianza.