Mwenyekiti wa Baraza la Magavana Ahmed Abdullahi amewasihi wataalamu wa Hazina ya Kitaifa kupunguza vikwazo vinavyochelewesha matumizi ya fedha zilizotengewa kaunti. Abdullahi alisema wakati mwingine kaunti hupokea mgao kwa wakati, lakini sheria za ununuzi huzuia matumizi ya wakati. Hii ni wakati Naibu Rais Kithure Kindiki amemwagiza Waziri wa fedha John Mbadi kukutana na magavana na timu zao za kiufundi wiki hii ili kushughulikia changamoto, ikiwa ni pamoja na upakiaji wa IFMIS, ujumuishaji kati ya mifumo ya IFMIS na KRA, na vikwazo vingine vinavyoathiri serikali za kaunti.

 

AHMED ABDULLAHI - AGREED