Naibu Rais Kithure Kindiki ameipongeza Hazina ya Kitaifa kwa kutoa fedha kwa wakati kwa kaunti, akisema serikali inatimiza ahadi yake ya kuondoa kucheleweshwa kwa malipo. Kindiki alisema mgao wote wa kila mwezi hadi kufikia Agosti umetolewa, bila kuacha malipo yoyote yanayosubiriwa na kuwezesha kaunti 47 kufadhili shughuli zao kwa ufanisi. Pia amempongeza Waziri wa fedha John Mbadi kwa kuwezesha utoaji wa haraka wa mgao wa kaunti.
KITHURE KINDIKI - MBADI