Hakimu Mkuu Mwandamizi wa Kangema aliyesimamishwa kazi ameshtakiwa kwa kupokea rushwa kufuatia uamuzi wa Mahakama Kuu ulioruhusu mashtaka yake kuendelea. Martin Kinyua Mutegi alifika mbele ya Mahakama ya Hakimu wa Kupambana na Rushwa pamoja na Afisa Mwandamizi wa Mashtaka na akakana mashtaka hayo. Aliachiliwa kwa dhamana ya shilingi elfu 800 au dhamana ya pesa taslimu shilingi elfu 400. Kesi hiyo itatajwa Septemba 7 kwa maelekezo zaidi.