Rais wa mstaafu Uhuru Kenyatta amepuuza madai kwamba anaingilia siasa za Kenya kwa kuwaunga mkono wawakilishi wa upinzani. Akizungumza jana, Uhuru alisema hana nia ya kutafuta nafasi yoyote ya kisiasa na ameridhika na fursa ambayo Wakenya walimpa ya kuitumikia nchi. Pia aliwasihi Wakenya kubaki na amani, umoja na heshima huku nchi ikijiandaa kwa Uchaguzi Mkuu wa 2027.
UHURU KENYATTA-DISMISS