Mwanamume mwenye umri wa miaka 35 alifariki baada ya kushambuliwa na kujeruhiwa na mbwa kadhaa wa mitaani alipokuwa akielekea nyumbani katika kijiji cha Githunguri, Kaunti ya Kiambu. Tukio hilo lilitokea yapata saa tisa alfajiri jumamosi. Kulingana na polisi, George Kimani alishambuliwa na mbwa kadhaa alipokuwa akielekea nyumbani. Binamu yake anaripotiwa kuwa alikutana na mbwa hao wakimshambulia mtu na kupiga mayowe, na kuwavutia umma, ambao waliitikia na kuwafukuza wanyama hao.