Takriban watu 40 wamefariki, na wengine 180 walipata majeraha katika ajali 33 za barabarani zilizoripotiwa kote nchini katika siku 20 za kwanza za mwezi huu wa Agosti, Shirika la Msalaba Mwekundu nchini limesema. Takwimu za hivi punde zinaashiria ongezeko la takwimu ambazo shirika hilo la kibinadamu lilitoa mapema mwezi huu, wakati liliripoti vifo 31 na majeraha 75 makubwa kutokana na ajali 23 katika siku 13 za kwanza za Agosti. Kulingana na Shirika hilo, data kutoka NTSA pia inaonyesha kwamba watu 2,150 walipoteza maisha yao katika ajali za barabarani kati ya Januari na Juni mwaka huu,