Katibu Mkuu wa zamani wa KNUT, Wilson Sossion anasema wakuu wa shule lazima waachilie vyeti vya KCPE na KCSE ambavyo vimezuiliwa kwa sababu ya karo ambayo haijalipwa. Sossion anasema wanafunzi hawapaswi kunyimwa vyeti vyao kwa sababu ya karo za shule ambazo hazijalipwa, akiongeza kuwa atahakikisha agizo hilo linafuatwa ikiwa watateuliwa kuwa kamishna wa Tume ya Huduma kwa Walimu. Alizungumza alipokuwa mbele ya Kamati ya Elimu ya Bunge kwa ajili ya kukaguliwa.
WILSON SOSSION - CERTIFICATES