Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta imewahimiza wagonjwa wanaotafuta huduma zisizo za dharura kuzingatia hospitali zilizo karibu nao huku idadi ya wagonjwa ikiongezeka kutokana na mgomo wa wafanyakazi wa afya unaoendelea katika kaunti kadhaa. Mkurugenzi Mtendaji wa KNH Dkt. Richard Lesiyampe anasema wimbi hilo limesababisha muda mrefu wa kusubiri na kucheleweshwa, hasa kwa huduma zisizo za dharura, huku hospitali hiyo ya rufaa ya kitaifa ikipata taabu kukabiliana na ongezeko la mahitaji.