Serikali inapanga kuagiza magunia milioni 25 ya mahindi ya kilo 90 ili kupunguza uhaba unaotarajiwa na kuzuia mgogoro wa chakula unaoweza kutokea kutokana na kupungua kwa uzalishaji katika maeneo makubwa yanayolima mahindi. Waziri wa Kilimo Mutahi Kagwe alisema mipango ya uagizaji huo tayari inaendelea, akiwahakikishia Wakenya kwamba Serikali ina hatua za kudumisha usambazaji wa chakula cha kutosha licha ya changamoto za uzalishaji zinazoikabili nchi.

MUTAHI KAGWE - IMPORT