Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro anatarajiwa kuanza kukipigia debe chama chake kipya cha People's Party of Kenya leo, akianza na ziara ya Kaunti ya Murang'a. Ziara hiyo inakuja siku moja baada ya kuzindua chama hicho na kutangaza kujiondoa kutoka chama tawala cha UDA ili kujiunga na upinzani.