Chama cha LSK kimelaani vurugu zilizotikisa ziara ya kisiasa ya Linda Mwananchi huko Homa Bay, kikiutaka mfumo wa haki kuwaadhibu waliohusika, kuwalipa fidia waathiriwa na kuwalinda Wakenya wanaotumia haki zao za kikatiba. Rais wa LSK Charles Kanjama alielezea matukio yaliyoshuhudiwa wakati wa shughuli za kisiasa kama vurugu mbaya zisizokubalika, kutovumiliana na uhuni wa kisiasa, akionya kwamba tabia kama hiyo haipaswi kuruhusiwa kuwa ya kawaida katika mazingira ya kisiasa ya Kenya.