Polisi mjini Kisumu wanawazuilia washukiwa 15 wa genge kufuatia operesheni iliyoongozwa na ujasusi kwenye ya barabara kuu ya Kisumu-Kericho. Wapelelezi walikamata magari matatu na kupata mapanga, visu, kamba, fimbo ya chuma na simu za mkononi. Washukiwa hao wanashughulikiwa kwa ajili ya kufikishwa mahakamani. Hata hivyo, wapelelezi bado wanamfuatilia mshukiwa kiongozi wa genge hilo, aliyetambuliwa kama Oliver Jaoko, almaarufu Oliveti, ambaye alitoroka kwa kuruka kupitia dirisha la gari wakati wa operesheni hiyo.