Kenya inachunguza kuanzishwa kwa sayansi na teknolojia ya nyuklia kwa wanafunzi wa shule za upili huku ikiimarisha elimu ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati (STEM) chini ya mfumo wa Elimu wa CBE. Akizungumza wakati wa mkutano wa kikanda jijini Nairobi uliohudhuriwa na wawakilishi kutoka nchi 10, Katibu wa Utafiti na Ubunifu Shaukat Abdulrazak alisema mageuzi ya mtaala yanapaswa kuwaweka wanafunzi katika sayansi ya nyuklia kabla ya chuo kikuu. Alibaini kuwa teknolojia ya nyuklia tayari inasaidia vipaumbele vya Kenya katika huduma ya afya, kilimo, rasilimali za maji na viwanda.

SHAUKAT ABDULRAZAK - NUCLEAR