Kampuni ya Kenya Airways imemteua Habil Waswani kama Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi kufuatia kujiuzulu kwa Kapteni George Kamal kutoka nafasi hiyo. Wasani, ambaye ni Katibu wa Kampuni ya shirika hilo la ndege na Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria, atachukua nafasi hiyo kuanzia Septemba 15. Kamal alijiuzulu kutoka nafasi yake kwa sababu za kibinafsi, lakini atabaki na shirika hilo kwa kipindi cha mpito cha siku 30 kabla ya kuondoka rasmi Septemba 30.