Beki wa Real Madrid Antonio Rüdiger ameamua kustaafu kutoka timu ya taifa ya Ujerumani ili kuzingatia klabu yake. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 ataweka kipaumbele uwezo wake wa kubaki na afya njema na kuichezea Madrid, ingawa mkataba wake wa sasa unaisha msimu ujao wa joto. Rüdiger alicheza mechi yake ya kwanza mwaka wa 2014, na akafanikiwa kuichezea Ujerumani mara 86.
Kufuatia mwanzo wao mbaya uliowashuhudia wakipoteza seti yao ya kwanza, katika ushindi wao wa 3-1 wa robo fainali ya ubingwa wa wanawake wa Afrika dhidi ya Algeria katika uwanja wa ndani wa Kasarani, kocha mkuu wa Malkia Strikers Geoffrey Omondi anasema watarekebisha makosa yao dhidi ya wapinzani wao Cameroon katika nusu fainali ya kesho. Omondi amewasihi mashabiki kuendelea kuwaunga mkono wanapotafuta kutetea taji lao na kujikatia nafasi katika michuano ya dunia ya mwaka ujao na nafasi ya Olimpiki ya majira ya joto ya Los Angeles mwaka 2028. Huyu hapa Omondi.
GEOFFREY OMONDI - MALKIA
Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Nairobi, Kajiado na Narok.
Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.