Mswada ulio mbele ya Bunge unalenga kuwalinda wafanyakazi na familia zao kutokana na uhamisho wa ghafla na usio wa haki wa kazi. Mswada wa Marekebisho wa Ajira wa Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa unawataka waajiri kuwaarifu wafanyakazi kuhusu sababu na matokeo ya uhamisho huo, na kupata idhini yao kabla ya kufanya hatua hiyo. Pendekezo hilo pia linalenga kuzuia uhamisho huo kutumiwa kama adhabu na kuimarisha haki ya wafanyakazi ya utendaji kazi wa haki.
DIDMUS BARASA - TRANSFER