Mhariri Mshirika wa Standard Group Alex Kiprotich amepatikana amewachwa kwenye kichaka huko Masinga, Kaunti ya Machakos, saa chache baada ya kudaiwa kutekwa nyara kando ya Barabara Kuu ya Gilgil–Nakuru. Watu waliompata wanasema alionekana amejeruhiwa na kutetemeka kabla ya kukimbizwa hospitalini kwa matibabu. Mazingira yaliyozunguka kutoweka kwake na jinsi alivyoishia Masinga bado hayajafahamika. Kampuni hiyo inasema tukio hilo linaweza kuhusishwa na majaribio ya kuwatisha ili wawanyamazishe, kufuatia utekaji nyara kama huo uliotibuka mwezi Juni.