Waajiri wanatoa wito wa kuchukuliwa kwa hatua za kisera ili kushughulikia uhaba wa ajira rasmi na marekebisho yanayosubiriwa kwa muda mrefu ya ushuru wa PAYE. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Waajiri Nchini Jacqueline Mugo anasema kupitia bendi za ushuru huo kutaweka huru nguvu ya matumizi ya Wakenya na kupunguza shinikizo la kifedha. Pia anaonya kwamba baadhi ya waajiri kwa sasa hawawezi kufuata sheria ya makato ya theluthi mbili ya Sheria ya Ajira kutokana na makato makubwa ya kisheria kutoka kwa mishahara ya wafanyakazi.


 

JACQUELINE MUGO – PAYE