Wizara ya Ardhi inalenga kutengeza takriban hati miliki 400,000 za ardhi chini ya mpango wake wa kitaifa unaoendelea wa umiliki, ikiwa ni pamoja na hati miliki za shule za msingi za umma. Waziri wa Ardhi Alice Wahome aliambia Seneti kwamba zoezi hilo linaendelea na akaahidi kuwasilisha ripoti ya maendeleo. Alisema gharama zote za upimaji na umiliki zimetimizwa kikamilifu na serikali.

ALICE WAHOME – PROGRAM