Gor Mahia itakabiliana na wenyeji Rayon sport katika fainali za CECAFA 2026 jijini Kigali, Rwanda Ijumaa, baada ya kuwashinda Al-Hilal ya Sudan kwa penalti 8-7, kufuatia sare ya 1-1 katika muda wa ziada. KO'gallo ilichukua uongozi kupitia bao la kujifunga la Steven Ebuela dakika ya 34, kabla ya Sudan kusawazisha kupitia Ansumana Samura na kupeleka mechi katika muda wa ziada. Wakati huo huo, Rayon iliishinda Jamus FC ya Sudan Kusini kwa mabao 3-1 katika mechi nyingine ya nusu fainali. Rayon iliishinda Gor 2-0 katika mechi ya kirafiki mwezi uliopita kabla tu ya cecafa kuanza.
Jua linashuhudiwa Isiolo,Marsabit na Samburu.
Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.