Baadhi ya viongozi wanaounga mkono serikali kutoka eneo la Magharibi wamekataa mapendekezo ya kumtaka Waziri wa Ushirika Wycliffe Oparanya kuwa mgombea mwenza wa Rais William Ruto katika uchaguzi mkuu ujao. Wakiongozwa na Gavana wa Bungoma Ken Lusaka, viongozi hao walisema pendekezo hilo ni mpango wa kugawanya eneo hilo na kugawanya kambi yake ya wapiga kura. Pia waliitaka serikali kuchukua hatua dhidi ya maafisa wanaodaiwa kutoa taarifa za siri kwa kiongozi wa DCP Rigathi Gachagua.

VOX POP-LEAD