Mbunge wa Mukurweini, John Kaguchia, alipelekwa kwenye makao makuu ya DCI kwa ajili ya kuhojiwa baada ya kukamatwa kwake. Kaguchia alikamatwa leo asubuhi nje ya studio za RMS jijini Nairobi baada ya kulala ndani ya jumba hilo usiku kucha. Mbunge huyo alidai polisi walikuwa wakimsubiri kumkamata kutokana na matamshi ya kisiasa yenye utata aliyotoa wakati wa mahojiano ya televisheni.